Tuesday, October 31, 2017

HDFA HANDENI

MAOMBI.


CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU WILAYA YA HANDENI HDFA.
P. O BOX 350
HANDENI. TANGA.
YAH: OMBI LA MAANDALIZI YA LIGI YA MWIKALO CUP.
Kwa Mwenyekiti na Katibu wa chama chetu cha mpira wa miguu wilaya ya Handeni, husika na somo hapo juu la maandalizi ya kiwanja cha michezo na mwaliko wa vilabu vya mchezo wa mpira wa miguu wilayani Handeni na wilaya za jirani.
Mwangalizi wa kampuni ya Biashara ya Mwikalo enterprise, Ndugu Haji Sedenga Mwikalo, amewaomba chama hicho cha HDFA kuandaa ligi hiyo ambayo inatazamiwa kuanza mwezi wa 12 mwaka 2017 wilayani hapo kwa mujibu wa mipango ya HDFA watakavyoipanga kulingana na taratibu zao za kiutendaji wa kimichezo wilayani hapo.
Sisi Mwikalo tupo tayari kimaandalizi na sasa tunasubiri maelekezo ya chama chetu cha HDFA kutupatia maelekezo ya kiwanja, timu zitakazo shiriki na mfumo wa ligi hiyo itakavyoandaliwa kimazingira ya kimichezo wilayani hapo…tutashukuru kwa msaada wenu.
Mwikalo cup, inatazamia kusimamia vifaa vya maandalizi… kama vile barua za mwaliko wa vilabu, barua za maombi ya viwanja au kiwanja, barua za mialiko ya viongozi ikibidi, barua za mawakala wa kuja kuangalia vipaji wilayani hapo na mengineyo.
ZAWADI.
Mpaka sasa, Mwikalo haijaweka wazi zawadi zitakazoandaliwa, lakini moja ya zawadi kubwa inayotarajiwa kwa timu zote ni kuja kwa mawakala wa michezo kuangalia wachezaji wa kusajiri katika vilabu vya ngazi za juu. Pia uhakika wa jezi za Mwikalo cup, pea moja itakabidhiwa kwa mshindi siku ya fainali, na bado tunatafakali mambo mengine yatakayotoa faraja kwa timu zetu.
Tunatanguliza shukurani zetu za dhati mapema kwa kutuongoza katika maandalizi haya ya mapema. Mwikalo ipo tayari kwa ushauri zaidi katika kuleta mafanikiyo haya ya kuendeleza michezo wilayani kwetu. Shukrani.
Mkurugenzi: Haji Sedenga Mwikalo.

0 comments:

Post a Comment