Tuesday, October 10, 2017

LIONEL MESSI ( FIFA WORLD CUP RUSSIAN 2018)

ARGENTINA.

Timu ya taifa ya Argentina imefuzu kushiriki katika mashindano ya kombe la dunia mwakani huko Urusi. Argentina ailikuwa inatafuta  nafasi ya kushiriki katika michuano hiyo ikicheza mchezo wao wa mwisho wa kutafuta nafasi ya kuendelea na mashindano ya kombe la dunia 2018 dhidi ya timu ya taifa ya Ecuador.

Mchezo huo ambao ulikuwa unaamua ni timu gani iendelee na mashindano hayo na timu gani ibaki, mpaka mwisho wa mchezo huo ilikuwa ni timu ya Argentina ikipata ushindi wa magoli 3 na timu ya Ecoudor wakipata goli 1.





Mchezaji wa timu ya Barcelona na timu taifa ya Argentina Lionel Messi aliibuka kuwa shujaa juu ya timu yake hii ni baada ya kuifungia magoli matatu muhimu katika mchezo huo.

Ecoudor ilikuwa nyumbani kuikaribisha timu ya Argentina. Argentina itaungana na timu zingine za taifa kama vile:-
  •  Misri.
  •  England.
  •  Brazil.
  •  Ureno.
  •  France 
Hizo ni baadhi ya timu zilizofuzu kushiriki kucheza kombe la dunia ( FIFA WORLD CUP RUSSIAN 2018)

0 comments:

Post a Comment